Skip to content
Entertainment

Man U Watoka Nyuma Na Kuwatandika Tottenham

BY Soko Directory Team · April 12, 2021 11:04 am

KEY POINTS

Manchester United walitoka nyuma kuibuka na ushindi wa mabao mawili kwa Moja dhidi ya Wapinzani wao Tottenham Hotspurs kutoka london inayofunzwa na Mkufunzi Mahiri Jose Mourinho.

Na Antonney Oduor

Manchester United walitoka nyuma kuibuka na ushindi wa mabao mawili kwa Moja dhidi ya Wapinzani wao Tottenham Hotspurs kutoka london inayofunzwa na Mkufunzi Mahiri Jose Mourinho.

Spurs walifungua ukurasa wa mabao kupitia Mkorea Son baada ya Bao la United kukataliwa pale ambapo Son alichezewa ndivyo sivyo. Kipindi cha pili kilianza na vishindo sanaa Kwani Mashetani wekundu walijawa mori kana kwamba walikuwa wamechanjwa chale.

Fred Rodriguez raia wa kibrazili alifunga bao lake la kwanza baada ya miaka mitatu, Edison Cavani alifunga la pili baada ya kupokea pasi murua kutoka kwa kinda Mason GreenWood aliyeingia katika nafasi ya Marcus Rashford katika dakika za lala salama.

Paul Pogba alikuwa katika ubora wake kwenye mechi Hiyo baada ya kutoa pasi ambapo Mason GreenWood alitia msumari wa Mwisho katika sanduku la Vijana wa Mourinho. Hii inaifanya United kushikilia nafasi ya Pili na alama sitini na tatu.

Alexandre Lacazette alikuwa Mchezaji wa Kumi wa katika orodha ya Arsenal kufikisha mabao hamsini katika mechi za Ligi Kuu Uingereza. Jana katika uga wa Bramal Lane washika bunduki wa Arsenal waliibuka na ushindi wa tatu bila ambao unawapeleka hadi Nafasi ya tisa katika jedwali.

Nahodha wao wa siku Lacazette alitia mabao mawili huku kinda wao wa kibrazili Gabriel Martineli kufunga Moja. Lacazette siku Ya Alhamisi alikashifiwa mno baada ya kukosa nafasi ya wazi walipokuwa wanacheza na Slavia Prague. Arsenal wanakusudiwa kucheza mechi ya na Prague ya marudiano.

Manchester City walifungwa na wachezaji kumi wa leeds mabao mawili kwa Moja. Westham wakaichapa Leicester City mabao matatu kwa mawili, Chelsea wakaigaragaza Crystal Palace mabao manne kwa Moja. Newcastle wakaichapa Wolves mabao mawili kwa Moja.

Kule Uhispania ni Kwamba miamba wa Catalunya Barcelona walicharazwa mabao mawili kwa Moja dhidi ya wapinzani wao Real Madrid. Kareem Benzema alifungua ukurasa wa mabao baada ya Toni Kroos kufunga la pili. Barcelona walipata bao la kufutia machozi kupitia Mchezaji wao Mingueza.

Athletico Madrid walitoka sare na Real Betis hivyo nasi kufanya nafasi yao ya kuongoza jedwali kuwa mashakani mno. Kwani wanaongoza jedwali hilo na alama Moja mbele.

Endelea kupata uhondo wa spoti Kwani wiki hii kutakuwa na sherehe ya Ndovu kumfanya mwanawe kitoweo.

Soko Directory is a Financial and Markets digital portal that tracks brands, listed firms on the NSE, SMEs and trend setters in the markets eco-system.Find us on Facebook: facebook.com/SokoDirectory and on Twitter: twitter.com/SokoDirectory

Trending Stories
Related Articles
Explore Soko Directory
Soko Directory Archives